Zaburi 105:39-42
39
Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
40
Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41
Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
42
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu, aliyompa Abrahamu mtumishi wake.