Zaburi 105:28-38
28
Alituma giza na nchi ikajaa giza, kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?
29
Aligeuza maji yao kuwa damu, ikasababisha samaki wao kufa.
30
Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.
31
Alisema, yakaja makundi ya mainzi, na viroboto katika nchi yao yote.
32
Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe, yenye umeme wa radi nchini yao yote,
33
akaharibu mizabibu yao na miti ya tini, na akaangamiza miti ya nchi yao.
34
Alisema, nzige wakaja, tunutu wasio na idadi,
35
wakala kila jani katika nchi yao, wakala mazao ya ardhi yao.
36
Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao, matunda ya kwanza ya ujana wao wote.
37
Akawatoa Israeli katika nchi wakiwa na fedha na dhahabu nyingi, wala hakuna hata mmoja kutoka kabila zao aliyejikwaa.
38
Misri ilifurahi walipoondoka, kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
Settings