Skip to content
Zaburi 105:1-7

Zaburi 105:1-7

1
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake, wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
2
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa, waambieni matendo yake yote ya ajabu.
3
Lishangilieni jina lake takatifu, mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
4
Mtafuteni Bwana na nguvu zake, utafuteni uso wake siku zote.
5
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
6
enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
7
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu, hukumu zake zimo duniani pote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options