Zaburi 103:6-13
6
Bwana hutenda haki, naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.
7
Alijulisha Mose njia zake, na wana wa Israeli matendo yake.
8
Bwana ni mwingi wa huruma na mwenye neema; si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo.
9
Yeye hatalaumu siku zote, wala haweki hasira yake milele,
10
yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.
11
Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia sana, ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha;
12
kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi.
13
Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha;
Settings