Zaburi 103:1-5
1
Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu.
2
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, wala usisahau wema wake wote,
3
akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote,
4
aukomboa uhai wako na kaburi, akuvika taji ya upendo na huruma,
5
atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema, ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
Settings