Skip to content
Zaburi 103:1-5

Ee Nafsi Yangu, Ubariki Bwana

Zaburi 103:1-5
1
Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu.
2
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, wala usisahau wema wake wote,
3
akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote,
4
aukomboa uhai wako na kaburi, akuvika taji ya upendo na huruma,
5
atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema, ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options