Skip to content
Zaburi 101:1

Zaburi 101:1

Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.
2
Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.
3
Sitaweka mbele ya macho yangu kitu kiovu. Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; hawatashikamana nami.
4
Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; nitajitenga na kila ubaya.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options