Mithali 8:5-11
5
Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili; ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.
6
Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema; ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.
7
Kinywa changu husema lililo kweli, kwa maana midomo yangu huchukia uovu.
8
Maneno yote ya kinywa changu ni haki; hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.
9
Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi; hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.
10
Chagua mafundisho yangu badala ya fedha, maarifa badala ya dhahabu safi,
11
kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.
Settings