Mithali 8:12-21
12
“Mimi hekima, nakaa pamoja na busara; ninamiliki maarifa na busara.
13
Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.
14
Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu; nina ufahamu na nina nguvu.
15
Kwa msaada wangu wafalme hutawala na watawala hutunga sheria zilizo za haki,
16
kwa msaada wangu wakuu hutawala, na wenye vyeo wote watawalao dunia.
17
Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
18
Utajiri na heshima viko kwangu, utajiri udumuo na mafanikio.
19
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi; kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.
20
Natembea katika njia ya unyofu katika mapito ya haki,
21
nawapa utajiri wale wanipendao na kuzijaza hazina zao.
Settings