Mithali 8:1-11
1
Je, hekima haitani? Je, ufahamu hapazi sauti?
2
Juu ya miinuko karibu na njia, penye njia panda, ndipo asimamapo;
3
kando ya malango yaelekeayo mjini, kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:
4
“Ni ninyi wanaume, ninaowaita; ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.
5
Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili; ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.
6
Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema; ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.
7
Kinywa changu husema lililo kweli, kwa maana midomo yangu huchukia uovu.
8
Maneno yote ya kinywa changu ni haki; hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.
9
Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi; hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.
10
Chagua mafundisho yangu badala ya fedha, maarifa badala ya dhahabu safi,
11
kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.
Settings