Skip to content
Mithali 7:6-12

Mithali 7:6-12

6
Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
7
Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
8
Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
9
wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
10
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
11
(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
12
mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options