Mithali 7:1-5
1
Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
2
Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3
Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
4
Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
5
watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
Settings