Mithali 3:5-12
5
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
8
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
Settings