Skip to content
Mithali 23:19-25

Mithali 23:19-25

19
Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima, weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.
20
Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo, au wale walao nyama kwa pupa,
21
kwa maana walevi na walafi huwa maskini, nako kusinzia huwavika matambara.
22
Msikilize baba yako, aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.
23
Nunua kweli wala usiiuze, pata hekima, adabu na ufahamu.
24
Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa, naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.
25
Baba yako na mama yako na wafurahi, mama aliyekuzaa na ashangilie!
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options