Mithali 23:12-16
12
Elekeza moyo wako kwenye mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13
Usimnyime mtoto adhabu, ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.
14
Mwadhibu kwa fimbo na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini.
15
Mwanangu, kama moyo wako una hekima, basi moyo wangu utafurahi,
16
utu wangu wa ndani utafurahi, wakati midomo yako itakapozungumza lililo sawa.
Settings