Rukia maudhui
Mithali 2:5-11

Chanzo na Thawabu ya Hekima

Mithali 2:5-11
5
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
6
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
9
Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
10
Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
11
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options