Mithali 13:4-9
4
Mvivu hutamani sana na hapati kitu, bali nafsi ya mwenye bidii hutoshelezwa kikamilifu.
5
Mwenye haki huchukia uongo, bali waovu huleta aibu na fedheha.
6
Haki humlinda mtu mwadilifu, bali uovu humwangusha mwenye dhambi.
7
Mtu mmoja hujifanya tajiri, kumbe hana chochote; mwingine hujifanya maskini, kumbe ana utajiri mwingi.
8
Utajiri wa mtu waweza kukomboa maisha yake, bali mtu maskini hasikii kitisho.
9
Nuru ya mwenye haki hungʼaa sana, bali taa ya mwovu itazimwa.
Settings