Mithali 12:24-28
24
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Settings