Mithali 1:24-27
24
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
25
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
26
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
Settings