Skip to content
Mithali 1:1-7

Mithali 1:1-7

1
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
2
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
3
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
4
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
5
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
6
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
7
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options