Filemoni 1:10-16
10
nakuomba kwa ajili ya mwanangu Onesimo, aliyefanyika mwanangu nilipokuwa kwenye minyororo.
11
Mwanzoni alikuwa hakufai, lakini sasa anakufaa sana wewe na mimi pia.
12
Namtuma kwako, yeye aliye moyo wangu hasa.
13
Ningependa nikae naye ili ashike nafasi yako ya kunisaidia wakati huu nikiwa kifungoni kwa ajili ya Injili.
14
Lakini sikutaka kufanya lolote bila idhini yako, ili wema wowote uufanyao usiwe wa lazima, bali wa hiari.
15
Huenda sababu ya yeye kutengwa nawe kwa kitambo kidogo ni ili uwe naye daima.
16
Si kama mtumwa, bali bora kuliko mtumwa, kama ndugu mpendwa. Yeye ni mpendwa sana kwangu na hata kwako zaidi, yeye kama mwanadamu na kama ndugu katika Bwana.
Settings