Rukia maudhui
Hesabu 9:1-5

Pasaka Yaamriwa huko Sinai

Hesabu 9:1-5
1
Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema,
2
“Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa.
3
Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”
4
Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka,
5
nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options