Hesabu 10:33-34
33
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
34
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.