Hesabu 1:5-19
5
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Settings