Skip to content
Mathayo 5:3-10

Mathayo 5:3-10

3
“Heri walio maskini wa roho, maana Ufalme wa Mbinguni ni wao.
4
Heri wale wanaohuzunika, maana hao watafarijiwa.
5
Heri walio wapole, maana hao watairithi nchi.
6
Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watatoshelezwa.
7
Heri wenye huruma, maana hao watapata rehema.
8
Heri walio na moyo safi, maana hao watamwona Mungu.
9
Heri walio wapatanishi, maana hao wataitwa wana wa Mungu.
10
Heri wanaoteswa kwa sababu ya haki, maana Ufalme wa Mbinguni ni wao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options