Skip to content
Mathayo 3:1-6

Mathayo 3:1-6

1
Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema,
2
“Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
3
Huyu ndiye yule aliyenenwa habari zake na nabii Isaya aliposema: “Sauti ya mtu aliaye huko nyikani, ‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’ ”
4
Basi Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia, akiwa na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
5
Watu walikuwa wakimwendea kutoka Yerusalemu, Uyahudi yote na nchi zote za kandokando ya Mto Yordani.
6
Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options