Mathayo 28:16-20
16
Basi wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda hadi Galilaya kwenye ule mlima ambao Yesu alikuwa amewaagiza.
17
Walipomwona, wakamwabudu; lakini baadhi yao wakaona shaka.
18
Yesu akawajia na kusema, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19
Kwa sababu hii, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu,
20
nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika mimi niko pamoja nanyi siku zote, hadi mwisho wa nyakati.”
Settings