Skip to content
Mathayo 27:26-31

Mathayo 27:26-31

26
Basi akawafungulia Baraba. Lakini baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
27
Kisha askari wa mtawala wakampeleka Yesu kwenye Praitorio na wakakusanya kikosi kizima cha askari kumzunguka.
28
Wakamvua nguo zake na kumvika vazi la rangi nyekundu, kisha
29
wakasokota taji ya miiba, wakaiweka kichwani pake. Wakamwekea fimbo katika mkono wake wa kuume, na wakapiga magoti mbele zake na kumdhihaki, wakisema, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
30
Wakamtemea mate, wakachukua ile fimbo wakampiga kichwani tena na tena.
31
Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakampeleka ili wakamsulubishe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options