Mathayo 25:3-8
3
Wale wapumbavu walichukua taa zao lakini hawakuchukua mafuta ya akiba,
4
lakini wale wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya akiba kwenye vyombo.
5
Bwana arusi alipokawia kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala.
6
“Usiku wa manane pakawa na kelele: ‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje mkamlaki!’
7
“Ndipo wale wanawali wote wakaamka na kuzitengeneza taa zao.
8
Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni mafuta yenu kidogo; taa zetu zinazimika.’
Settings