Skip to content
Mathayo 20:30-34

Mathayo 20:30-34

30
Vipofu wawili walikuwa wameketi kando ya barabara. Waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie!”
31
Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, tuhurumie.”
32
Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
33
Wakamjibu, “Bwana, tunataka kuona.”
34
Yesu akawahurumia na kuwagusa macho yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao wakamfuata.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options