Mathayo 14:6-10
6
Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode,
7
kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba.
8
Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.”
9
Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake.
10
Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani.
Settings