Mathayo 10:9-13
9
Msichukue dhahabu, wala fedha, wala shaba kwenye vifuko vyenu.
10
Msichukue mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala jozi ya pili ya viatu, wala fimbo, kwa maana mtendakazi anastahili posho yake.
11
“Mji wowote au kijiji chochote mtakapoingia, tafuteni humo mtu anayestahili, nanyi kaeni kwake mpaka mtakapoondoka.
12
Mkiingia kwenye nyumba, itakieni amani.
13
Kama nyumba hiyo inastahili, amani yenu na iwe juu yake. La sivyo, amani yenu na iwarudie ninyi.
Settings