Marko 13:33-37
33
Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia.
34
Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.
35
“Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko.
36
Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala.
37
Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’ ”
Settings