Luka 8:51-56
51
Walipofika nyumbani kwa Yairo, hakumruhusu mtu yeyote aingie ndani naye isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, pamoja na baba na mama wa yule binti.
52
Wakati ule ule watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili ya huyo binti. Yesu akawaambia, “Acheni kulia. Huyu binti hajafa, ila amelala.”
53
Wao wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekwisha kufa.
54
Yesu akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!”
55
Roho yake ikamrudia, naye akainuka mara moja. Akaamuru apewe kitu cha kula.
56
Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote juu ya yale yaliyotukia.
Settings