Luka 5:27-32
27
Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
28
Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
29
Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
30
Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
31
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
32
Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
Settings