Rukia maudhui
Luka 4:16-21

Yesu Ahubiri Nazareti

Luka 4:16-21
16
Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
17
naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
18
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
19
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
20
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
21
Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options