Skip to content
Luka 24:36-41

Luka 24:36-41

36
Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
37
Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka.
38
Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu?
39
Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
40
Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
41
Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options