Skip to content
Luka 23:50-54

Luka 23:50-54

50
Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
51
lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
52
Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53
Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
54
Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options