Skip to content
Luka 10:25-28

Luka 10:25-28

25
Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”
26
Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
27
Akajibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ ”
28
Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options