Luka 1:68-74
68
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,
71
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
Settings