Walawi 11:14-22
14
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
15
aina zote za kunguru,
16
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
17
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
18
mumbi, mwari, nderi,
19
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
20
“ ‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
21
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
22
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
Settings