Maombolezo 5:1-5
1
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
2
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
3
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
4
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
5
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
Settings