Maombolezo 3:63-66
63
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
64
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
65
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
66
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.