Maombolezo 3:55-58
55
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
56
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
57
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
58
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.