Maombolezo 3:2-9
2
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
3
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
4
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
5
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
6
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
7
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
8
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
9
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
Settings