Skip to content
Maombolezo 3:1-6

Maombolezo 3:1-6

1
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
2
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
3
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
4
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
5
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
6
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options