Skip to content
Waamuzi 5:19-22

Waamuzi 5:19-22

19
“Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
20
Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
21
Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
22
Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options