Skip to content
Waamuzi 12:8-15

Waamuzi 12:8-15

8
Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
9
Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
10
Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
11
Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
12
Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
13
Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
14
Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
15
Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options