Skip to content
Waamuzi 11:4-8

Waamuzi 11:4-8

4
Baada ya muda Waamoni wakafanya vita na Israeli,
5
viongozi wa Gileadi wakaenda kumchukua Yefta katika nchi ya Tobu.
6
Wakamwambia Yefta, “Uwe jemadari wetu, ili tuweze kupigana na Waamoni.”
7
Yefta akawaambia, “Je, hamkunichukia mimi na kunifukuza katika nyumba ya baba yangu? Kwa nini mnanijia sasa, wakati mna matatizo.”
8
Viongozi wa Gileadi wakamwambia Yefta, “Lakini sasa tumegeuka kukuelekea wewe, ili uende pamoja nasi kupigana na Waamoni, nawe utakuwa kiongozi wetu juu ya watu wote wa Gileadi.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options