Yohana 7:45-49
45
Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
46
Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
47
Mafarisayo wakajibu, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48
Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
49
Lakini huu umati wa watu wasiojua Sheria ya Mose, wamelaaniwa.”
Settings