Yohana 5:10-12
10
Kwa hiyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato, si halali wewe kubeba mkeka wako.”
11
Yeye akawajibu, “Yule mtu aliyeniponya aliniambia, ‘Chukua mkeka wako na uende.’ ”
12
Wakamuuliza, “Ni mtu gani huyo aliyekuambia uchukue mkeka wako uende?”